NHC wazindua zoezi la uuzaji viwanja wilayani Chato
Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com
Wananchi na
wawekezaji mbalimbali wametakiwa kuchangamkia fursa ya uuzaji viwanja zaidi ya
elfu moja vya makazi na biashara katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani
Geita ambavyo tayari vimepimwa katika Kata ya Muungano.
Akizungumza
jana kwenye uzinduzi wa zoezi la uuzaji wa viwanja hivyo, Mkurugenzi wa Shirika
la Nyumba la Taifa (NHC), Dkt. Maulid Banyasi alisema zoezi hilo linasimamiwa
na NHC kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chato.
Naye Mkuu wa
Wilaya Chato, Mtemi Msafiri alishauri kuundwa Kamati Maalum ya uuzaji wa
viwanja hivyo hatua itakayosaidia kuondoa malalamiko ikiwemo baadhi ya watu
kupata viwanja vingi huku wengine wakikosa.
Na Joel Maduka, Geita
Tazam BMG Online TV hapa chini
Tazam BMG Online TV hapa chini
No comments: