LIVE STREAM ADS

Header Ads

ILEMELA- Zahanati ya Lukobe kuleta ahueni kwa wananchi

Yaliyomo humu (Habari, Matangazo na Maoni) si msimamo wa Binagi Media Group. Mawasiliano 0757 43 26 94 ama binagimediagroup@gmail.com

Kukamilika kwa ujenzi wa Zahanati ya Lukobe iliyopo Kata ya Kahama wilayani Ilemela, kunatarajia kuleta ahueni ya upatikanaji wa huduma za afya kwa wakazi wa Mtaa wa Lukobe ambao wamekuwa wakitembea umbali mrefu hadi kilomita 10 kusaka huduma za afya.

Mradi huo uliofunguliwa na Kiongozi wa mbio za Mwenge kitaifa jumapili Mei 19, 2019 ni miongoni mwa miradi 10 iliyopitwa na Mwenge wilayani Ilemela ambapo ujenzi wake ulianza baada ya kuibuliwa na wakazi wa Mtaa wa Lukobe na kuungwa mkono na Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela pamoja na mfadhili kutoka nchini Canada, Dawn Shaller.
Tazama BMG Online TV hapa chini

No comments:

Powered by Blogger.