Uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza Uko katika Ukarabati wa Hali ya Juu ikiwa ni katika Kutii agizo lililotolewa na TFF kwa Wamiliki wa Uwanja huo ambao hali yake ilikuwa dhoofu na hivyo kupelekea Mechi mbalimbali kupigwa Stop katika Uwanja Huo. Maeneo ambayo yalikuwa taani uwanjani hapo ambayo yanafanyiwa Ukarabati ni pamoja na Vyoo, Bafu na Vyumba vya Kubadilishia nguo. Pichani ni Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza Joyce Masunga akizungumza na Waandishi wa habari jana Ijumaa kabla ya Kutembelea Uwanja huo ili kujionea ukarabati unaoendelea ambao ulianza Jumatatu Wiki iliyoisha. |
No comments: